Mchezaji sugu wa Arsenali ataja mpango wake wa kuelekea Barcelona

September 2024 ยท 1 minute read

- Mchezaji maarufu katika timu ya Arsenali, Hector Bellerin amesema kuwa angefurahi sana kurudi Barcelona

- Kulingana na Bellerin, akipewa nafasi ya kurudi Barcelona ataiacha Arsenali papo hapo

Mlinzi katika timu ya Arsenali, Hector Bellerin amesema kuwa anao msukumo wa kurejea Barcelona, timu iliyoshinda kombe la mabingwa nchini Uhispania.

Habari Nyingine: Ni nani kama mwanamume huyu? Tazama alichomfanyia mkewe

Bellerin mwenye umri wa miaka 23 kutoka Uhispania anahiari kurudi Barcelona aliyoiacha mwaka wa 2011, na kuiacha Arsenali akipata tu nafasi.

Habari Nyingine: Huyu ndiye kijana maarufu anayemkosesha usingizi bintiye Akothee (picha)

Licha ya kuwa na nia ya kuelekea Barcelona, kuna vilabu vingine Uingereza vinavyomfuatilia kwa karibu kama vile Chelsea, Juventus na Inter Millan, ambazo zitataka huduma za mchezaji huyo.

Habari Nyingine: Picha za bintiye Gideon Moi ni thibitisho kwamba ni mrembo kupindukia

Akisema hayo, Bellerin alikariri kuwa kandanda hugeuka na kwa sasa anafurahia soka ya Uingereza ambapo ameishi miaka saba sasa lakini baadaye akipewa nafasi ya kurejea Uhispania, atafungasha virago tu.

"Usoni, huwezi jua. Bila shaka nimekua nikiwa Barcelona na kila saa nikiwaona wakicheza, nawatakia ushindi," Alisema.

Read ENGLISH VERSION

Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke , kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibIB0gJFmpJygla%2Buq7WMrKygrV2srm6t0aycp5mcnnqiwMCjmGaloJa7qLuMsJiknV2srm631J6jnqOVlnqjrdGcnKWnnpZ7qcDMpQ%3D%3D